
Kampeni kubwa ya kuondoa viuatilifu hatari vinavyotumika katika kilimo yazinduliwa Afrika Mashariki
Mpango mpya wa kikanda wa miaka mitatu wa kupunguza matumizi ya viuatilifu vyenye hatari kubwa (HHPS) umezinduliwa Afrika Mashariki, mafanikio makubwa katika usalama wa chakula na ulinzi wa mazingira. Jitihada hii, inayofadhiliwa na Global Chemicals Framework (GFC) Fund of the United Nations Environment Program (UNEP), inaunganisha Tanzania, Kenya na Ethiopia katika juhudi ya pamoja ya kuwabadilisha wakulima kwenda kwenye mbinu za kilimo endelevu.